CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeibua tuhuma nzito za ufisadi wa mabilioni ya fedha, kikidai kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), hasa kupitia makundi ya wasaka urais, kimeanza kutumia mbinu haramu kutafuna fedha za Watanzania kwa ajili ya kampeni za 2015, kwa namna ile ile iliyotumika kufanikisha wizi wa EPA, wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 2005. ...
Chama Cha Mapinduzi (CCM) tawi la Afrika kusini kupitia Mwenyekiti wake Ndugu, Kelvin Nyamori, kimetoa taarifa za kusikitishwa na Habari zilizochapishwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, (tovuti yetu dada, JamiiForums ikiwa mojawapo) juu ya utapeli uliofanywa na aliyekuwa katibu wa CCM wa tawi hilo, Ndugu Paul Pius Albino Mkoba, wenye thamani ya Shilingi Millioni 37 za Kitanzania (RAND 200,000) ...
Leo tarehe 27 Machi 2013 ilikuwa siku nyingine ambapo wanahabari wameshindwa kufikia muafaka juu ya suala la usalama wao. Mjadala huu uliandaliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT) lengo likiwa ni kutafuta mbinu ya kujilinda hususani baada ya kushambuliwa kwa mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Absalom Kibanda. Mada ilikuwa “Usalama wa Waandishi wa Habari Tanzania” ...